Latest Stories

Subscription

You can subscribe to Red Carpet by e-mail address to receive news and updates directly in your inbox. Simply enter your e-mail below and click Sign Up!

TOP 5 Most Popular Post

    Popular Posts

    theudaku

    Ads

    Powered by Blogger.

    Recent Posts

Recently Comments


News

News


WAKATI Wizara ya Afya kupitia shirika linalotoa huduma ya Elimu ya Afya la PSI wakiwa wameibuka na kampeni ya Tupo Wangapi? Tulizana kwa ajili ya kupunguza kasi ya maambukizi ya Ukimwi, Ijumaa limenasa mtungo hatari wa ngono baada ya picha za njemba moja (jina tunalo) kubambwa zikimuonesha ikiliwazwa kimahaba na takriban wanawake 12.
Imefahamika kuwa picha hizo zinazomuonesha jamaa huyo akijiliwaza zilipigwa hivi karibuni kwenye nyumba moja iliyopo Mbezi Beach pembezoni mwa Bahari ya Hindi.
NI WASICHANA WADOGO
Kwa mujibu wa picha hizo, baadhi ya mademu hao ni wadogo lakini wanajua mambo ya kikubwa kwa namna walivyokuwa wakijiachia na mwanaume huyo.
Aidha, chanzo chetu kinacholifahamu tukio hilo kwa undani kilitutonya kuwa, mchezo mzima ulikuwa ni kwamba akimaliza ‘kucheza’ na mmoja alikuwa akimfuata mwingine na kujisevia.

NI TUKIO GANI?
Kwa mujibu wa chanzo hicho, ilikuwa ni sehemu ya sherehe iliyoandaliwa na mtoto wa kigogo mstaafu wa serikali iliyopewa jina la pati ya kula bata.
Ilidaiwa kuwa jamaa huyo alitimba kwenye pati hiyo na wasichana kibao ambapo baada ya kukolea kinywaji, ndipo hali ikabadilika ikawa kama Sodoma na Gomora.
“Alianza kwa kucheza nao kwenye bwawa la kuogelea baadaye wakatoka na kuendeleza michezo ya kikubwa pembeni. Kwa kweli hii ni aibu kwa taifa,” kilisema chanzo hicho.
AWALIPA LAKI MOJA
Ilidaiwa kuwa baada ya kumridhisha mademu hao walilipwa shilingi laki moja kila mmoja jambo ambalo lilithibitishwa na mmoja wao aliyetajwa kwa jina moja la Salama.
SOO LATINGA POLISI
Habari za kuaminika za kipolisi zilieleza kuwa baada ya picha hizo kuzagaa kwenye mitaa mbalimbali jijini Dar, hatimaye soo lilitinga katika Kituo cha polisi cha Kawe ambapo baadhi yao walitiwa nguvuni na baadaye kuachiwa kwa dhamana.
TULIZANA, TUKO WANGAPI?
Tukio la njemba huyo na wasichana hao linalenga kutia doa kwenye kampeni ya Tupo Wangapi? Tulizana ambayo lengo lake kuu ni kuhakikisha ngono za mnyororo zinakwisha ili kuinusuru jamii na ugonjwa hatari wa Ukimwi.
Ngono za msururu maarufu kwa jina la mtungo huanzia kwenye tamaa ya mtu mmoja kutaka kufanya mapenzi na watu wengi huku wale ‘anaoshea’ nao wakiwa na wapenzi wengine hivyo jamii inapaswa kuacha tabia hiyo mara moja.
Posted in: | Saturday, June 9, 2012